inaendelea, sambamba na mwamdishi Late, Mwl. Godwin Dihigo. Je fundisho la kuridhi Dhambi wachungaji wamelipata wapi? Uwenda pengine wachungaji wengi hawajaelewa fundisho lililopo katika Kuto 20: 4-6 Lakini hawajaelewa au khawataki kuwaambia ukweli washirika wao juu ya maana ya fundisho lililopo Kuto 20:5-6 katika mlango huo Mungu anasema Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilichojuu mbinguni wala kilicho chini duniani wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia kwa kuwa mimi Bwana Mungu wako ni Mungu mwenye wivu nawapatiliza wana uovu wa Baba zao Kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao. Nami nawarehemu maelfu Elfu wanipendao na kuzishika amri zangu. Manabii, wachungaji na Waalimu wa uongo uwafundisha kuwa watu wanaweza kurithi dhambi za Baba zao kwa sababu Mungu amesema anawapatiliza Watoto kizazi cha tatu mpaka kizazi cha nne kwa maovu ya Baba zao. Kwa wale wasiochunguza maandik...