Ruka hadi kwenye maudhui makuu

DHAMBI YA MAAGANO (LAANA YA UKOO) part 03


 inaendelea, sambamba na mwamdishi Late, Mwl. Godwin Dihigo.

Je fundisho la kuridhi Dhambi wachungaji wamelipata wapi?

 

Uwenda pengine wachungaji wengi hawajaelewa fundisho lililopo katika Kuto 20: 4-6

 

Lakini hawajaelewa au khawataki kuwaambia ukweli washirika wao juu ya maana ya fundisho lililopo Kuto 20:5-6 katika mlango huo Mungu anasema

Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote  kilichojuu mbinguni wala kilicho chini duniani wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia kwa kuwa mimi Bwana Mungu wako ni Mungu mwenye wivu nawapatiliza wana uovu wa Baba zao Kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao. Nami nawarehemu maelfu Elfu wanipendao na kuzishika amri zangu.

 

Manabii, wachungaji na Waalimu wa uongo uwafundisha kuwa watu wanaweza kurithi dhambi za Baba zao kwa sababu Mungu amesema anawapatiliza Watoto kizazi cha tatu mpaka kizazi cha nne kwa maovu ya Baba zao.

 

Kwa wale wasiochunguza maandiko kwao ni rahisi kuwaambia wachungaji wao sawa kabisa pale wanapoambiwa wawe na maombi maalumu na sadaka maalumu kuondoa laana au dhambi hiyo.

 

Nakata ujuwe sasa.

 

Yapo mambo mawili ya kuelewa katika mistali hii.

 

1. Mungu anawapatiliza Watoto hao tu nao ni wale wanaomchukia Mungu katika maagizo yake yaliyosema. Wale wanaowatii wazazi wao kwa kufanya dhambi kama zile wanazofanya wazazi wao.

 

Kwa mfano Baba anamwambia Mtoto wake lazima unywe pombe kama mimi ili nikifa wewe utachukua urithi wa tabia zangu nk. Huyu Mtoto anapokubali kuchukua maovu yote ya Baba yake anamchukia Mungu.

 

2. Hata kama ilikuwa ndivyo ilivyokuwa Mungu aliwaambia Waislaeli atawapaliza wana uovu wa Baba zao kizazi cha tatu na cha nne. Je mpaka leo ni kizazi cha ngapi tangu aliposema?

 

Hii ni kuonyesha kuwa wachungaji wengi wanawapoteza sana wanadamu wenzao.

 

Katika 2Nyak tunathibitisha hili kutoka katika Neno la Mungu. Tazama 2Nyak 25:1-4 maneno yanasema.

 

Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala akatawala katika Yerusalemu miaka ishirini na kenda na Jina la Mamaye aliitwa Yehoadan wa Yerusalemu akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, lakini si kwa moyo mkamilifu. Basi ikawa alipopata nguvu katika ufalme wake, akawaua wale waliomuua mfalme Babaye. Lakini watoto wao hakuwaua ila alifanya sawa sawa na hayo yaliyoandikwa katika Torati katika kitabu cha Musa kama Bwana alivyoamuru, akisema: Mababu wasife kwa makosa ya wana wala wana wasife kwa makosa ya Mababa. Lakini kila mtu atakufa kwa dhambi yake mwenyewe.

 

Swali ambalo watu wangejiuliza.

Wamepata wapi habari ya watu kurithi dhambi ya ukoo? Yaani mababu wametenda dhambi watoto na wajukuu wakarithi dhambi zao?

 

Sijui kama hii elimu ni ya kiroho kweli, Amazia anasema akawauwa wale watumishi wa mfalme baba yake lakini watoto wao hakuwaua, kwa sababu Mungu amesema hakuna mtu awezaye kurithi dhambi ya mtu mwingine.

 

Basi hawa wasemao kuna dhambi ya ukoo ni watumishi wa shetani Mungu wa ulimwengu huu.

itaendelea................

 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...