Ruka hadi kwenye maudhui makuu

THE PARADISE LOVE (usiyoyajua kuhusu mahusiano) part 4


 

Yapo Mambo mawili ya kufanya kabla ya mahusiano (uchumba)

siku zilizopita tuliona jambo la kwanza ni MUNGU. leo inaendelea na jambo la pili kama ifuatavyo;

2. Kuwa katika uhalisia wako

“…Mimi unielewe tu kuwa Nina wivu Sana, yani Sana tu sipendi kuona unatumia muda mwingi na wengine. Ila najua nakupenda Kwa dhati ndio maana nakuwa hivyo. Nisamehe pale ninapokosea.”

Kipindi cha uchumba au kutafuta mwenza ni kipindi cha maandalizi ya maisha ya mapenzi hasa ndoa. Ni kipindi ambacho jinsi ulivyo na namna unavyoenenda vitaweza kumshawishi au kumvutia mtu kwako. Jambo kubwa linalokosewa kipindi hiki ni kuigiza tabia au maisha fulani ili uonekane bora zaidi. Hali hii husababisha kuwepo Kwa mahusiano yasiyo na uhalisia, mahusiano ya maigizo ambayo huunganisha watu wawili wasio sahihi.

Kijana aliye na imani na Mungu na anayeongoza maisha yake kwa msaada wa Mungu hawezi kuigiza mwenendo wake wa maisha, unatakiwa kuwa wewe na uoneshe tabia zako na misimamo yako ambayo umejiwekea katika maisha yako. Kama hupendi kuvaa nguo ndefu basi kuwa hivyo, Kama hupendi kwenda club kuwa hivyo, Kama unapenda kutoka mara kwa mara kuwa hivyo, kama hupendi kula chakula Fulani basi kuwa hivyo ijulikane (ufunuo 3; 15-16). Ukiwa katika uhalisia wako kipindi hiki itakusaidia kupata mtu sahihi ambaye ataweza kukubaliana na tabia na mapungufu yako na wote kwa pamoja mtafanikiwa katika maisha yenu. Ukiwa katika uhalisia wako itakusaidia kuwa na maisha mepesi, hutatumia nguvu nyingi kuishi na mwenza wako kipindi cha uchumba hata ndoa hapo baadae ambayo ndio paradise inayotazamiwa. Kila mmoja akiwa katika uhalisia wake, itakuwa rahisi kujua udhaifu wa mwenzi wake na ni vipi ataukamilisha udhaifu huo kwa ajili yake, atatambua ni wapi nguvu ya mwenzi wake ilipo ili pia aweze kuitumia kukamilisha mapungufu yake na kuleta mafanikio.

Ukiwa katika uhalisia wako, utapunguza na kuondoa lawama zisizo na msingi katika maisha yako na ya mwenzio, utajenga mahusiano bora ambayo msingi wake ni Mungu na kweli. Ukiwa katika uhalisia wako utatambua mahali pa kuboresha pale utakapoona nia na haja ya mabadiriko katika maisha yako, ukiwa wewe utampendeza Mungu na kuzuia dhambi mbalimbali zinazotokana na udanganyifu. Lengo la mahusiano ni kuandaa paradise ambayo ni ndoa, mkiwa wakweli itakuwa rahisi kwenu wawili kuwa na pumziko la moyo. Hutoweza kuwaza mabaya juu ya mwenzi wako kwakua unamfahamu alivyo, mambo anayoweza na asiyoweza kufanya.

itaendelea.......

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...