Ruka hadi kwenye maudhui makuu

THE PARADISE LOVE (Usiyoyajua Kuhusu Mahusiano) part 3


Yapo Mambo mawili ya kufanya kabla ya mahusiano (uchumba).

1. Mungu kwanza

“Mungu yu nami atanisaidia…. Mimi naamini maono yangu yatatimia tu ilimradi nayafanyia kazi na nayaombea, yatatimia. Hata nikifa kesho ninauhakika utawaadithia watu kwamba nilijitahidi kukuonesha upendo wa dhati…”

Mara nyingi watu wanaishi Kwa mazoea nikimaanisha huishi kulingana na mazingira au siku husika inavyotaka waishi. Ukiwa Kama mwanadamu aliyekamilika unapaswa kuwa na ndoto, mawazo na mipango mbalimbali vitakavyo kusaidia kuishi vyema duniani. Jambo moja ambalo linatakiwa kuwa katika mipango yako ni kuhusu mwenza wako, unahitaji mwenza wa aina gani, kutoka familia gani, mwenye tabia gani n.k.

Hili jambo ni muhimu sana katika maisha yako, ingawa utajiwekea orodha ya tabia, muonekano na chimbuko la mtu umtakaye ila bado sisi ni wanadamu na tunaupeo wa kibinadamu. Pengine mawazo tuliyonayo hayatatufaa baadae au tabia na matakwa tuliyojiwekea havitatukuza na kutupatia maisha bora baadae hivyo tunamuhitaji Mungu kutusaidia katika maamuzi na machaguo yaliyosahihi. (Mithali 9; 10). Mungu wetu ni Mungu wa maarifa, Mungu mwenye hekima iliyozidi viumbe vyote. Mungu hutuwazia mema kila siku na anatujua tangu tumboni mwa mama zetu. Katika mipango yote tunayojiwekea mwenye kuikamilisha ni Mungu. (1wakorintho 2; 6-7).

 

Ukitaka upate kile unachokihitaji lazima ujikite katika maombi kila wakati, maombi yatakusaidia kuchambua vigezo ulivyo jiwekea na kuboresha zaidi. Mungu kupitia maombi atakupa hekima ya kuchagua mwenza sahihi wa maisha yako, tujikite katika kusali kila wakati, tumtangulize Mungu kwanza na kila kitu kitaenda sawa.

Hakuna muujiza utakaotokea kama mtu kuibuka tu kwako bila mipango na maombi, yeye baba aliye juu atakuwezesha kuchagua mtu sahihi kati ya wale wote utakaowaona kwenye maisha yako. Wakati mwingine utaona umechagua mwenza ambaye ana tabia moja au mbili tu au hana kabisa kati ya zile ulizojiwekea kama vigezo ila jua kama Mungu akiwa ndani yako utakuwa mahali salama na umepata mtu sahihi.

Katika wakati wa machaguzi unatakiwa kuwa mpole na usiyekuwa na haraka. Mungu wetu ni Mungu wa ustadi, hakurupuki. Tumia muda wako vizuri katika kuchunguza upande wa pili na kuvumbua kama kweli anakitu ndani yake ambacho Mungu anasema nawe katika hilo. Binadamu tulio wengi tunatabia ya kuigiza tabia Fulani pale tunapohitaji kitu, ukimshirikisha Mungu ukachukua muda utaweza kujua undani wa mtu na umuhimu au ubora wake.

itaendelea......


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...