Ruka hadi kwenye maudhui makuu

THE PARADISE LOVE (usiyoyajua kuhusu mahusiano) part 2


Na Samwel Dihigo.

Mahusiano ya kimapenzi

Dhumuni langu sio kuzungumzia mahusiano kwa ujumla bali ni kujikita katika mahusiano ya kimapenzi ambayo kwa upana zaidi yamekuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Katika maisha yangu hapa duniani mpaka sasa nimeshuhudia watu wengi wakiteseka katika aina hii ya uhusiano, wengine wamekufa, wengine hawana amani, wengine wamepoteza nafasi kubwa sana n.k. Mahusiano ya kimapenzi yamekuwa chanzo cha marumbano, uharifu, machukizo, vilio na visasi, mahusiano hayana tena upendo na uimara kama hapo awali.

Kwa kipindi hiki, mahusiano mengi yanaishia njiani na watu kufarakana, yale ambayo yanapata nafasi ya kuwa hai basi yanakuja kufa kipindi cha ndoa na kufanya maisha ya ndoa kuwa mabaya na kukera. Nimeshuhudia kwa ukubwa watu wakiwalalamikia wenza wao kwenye ndoa na kuwashauri vijana kutothubutu kuolewa au kuoa kwasababu ndoa zao zimekuwa kama jehanamu ya moto. Sisemi kwamba mimi ni bora sana katika hili na ndio maana nimeamua kuandika hili la!, nimeamua kufanya uchunguzi na kuja na majibu ambayo kwa upeo wangu naona yataweza kusaidia katika kufumbua watu macho, kuwasaidia kuimarisha mahusiano yao na kuwawezesha kufikia ndoa, si ndoa tuu bali ndoa yenye upendo na furaha, ndoa tunayo ifananisha kama paradise au pepo.

Mahusiano ya kimapenzi yapo katika hali mbili, moja ni uchumba na mbili ni ndoa. Katika hali zote mbili kuna mambo muhimu ya kufanya ili kuimarisha kote, ndoa bora inatokana na mahusiano bora ya uchumba ambayo yamefuata hatua kadhaa na kufanya mambo kadhaa, na mambo hayo yanakwenda kuimarika zaidi kipindi cha ndoa. Kutokana na hilo nimeona wazi katika kitabu hiki kuelezea mambo muhimu ya kufanya au kuanza nayo kabla hujapata mwenza au kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi na mtu, na ni mambo yapi ya kuyafanya baada ya kumpata mtu sahihi wa maisha yako (uchumba), na kwa ujumla mambo yote hayo yatasaidia kuimarisha na kutengeneza mahusiano bora na kuandaa ndoa njema hapo baadae ambayo ndio paradise tunayo itazamia. Ndoa haipaswi kuwa kama jela au jehanamu ya moto, mahusiano au uchumba pia hayaitajiki kuwa chanzo cha maumivu na majuto baina ya watu, watu wote kwa pamoja wakitimiza wajibu wao basi watatengeneza mahusiano imara, bora, yenye furaha na ndoa njema hapo baadae.

Kuna mambo nane muhimu ya kufanya ili kufanikisha mahusiano mema ya kimapenzi baina ya watu wawili, mambo hayo ni; Mungu kwanza, kuwa katika uhalisia wako, mawasiliano, kujitoa, hudumia, usijilinganishe, upendo, mguso wa kimwili. Ungana nami katika kuelezea mambo haya na naamini yatakwenda kukusaidia.

itaendelea.........

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...