Ruka hadi kwenye maudhui makuu

THE PARADISE LOVE (Usiyoyajua Kuhusu Mahusiano) SEHEMU YA 01


Mahusiano ni nini?

Maisha ya mwanadamu hapa duniani yanategemea Sana uwepo wa mtu mwingine, na ndio maana watu husema sisi binadamu tuna tegemeana kwa Nyanja nyingi sana ili kufanikisha mambo mengi ya kila siku. Mfano:, ninamuhitaji dereva wa daladala kunifikisha sehemu ninayohitaji kila siku, ninamuhitaji mwalimu ili kunifundisha na kuniongoza kupata maarifa katika maisha, ninamuhitaji mlinzi ili kuweka mali zangu salama. Utegemeano huu kati ya mtu na mtu ndio hupelekea kutokea kwa mahusiano.

Mahusiano ni hali inayotokea pale mtu anapokuwa karibu na mtu mwingine katika muundo fulani, wakishirikiana na kutegemeana katika mambo mbalimbali, hali hii huleta ushirikiano wa kiakili, kihisia, na hata kimwili kulingana na uhusiano wao ulivyo.  Mahusiano yanaweza kuwa kati ya ndugu na ndugu, rafiki kwa rafiki, familia kwa familia, nchi kwa nchi n.k. Ijapokuwa mara nyingi ukizungumzia neno mahusiano watu wanakimbilia kwenye mahusiano ya kimapenzi bila kujua kuwa kuna aina nyingi sana za mahusiano kulingana na sehemu na wakati. Zipo aina kuu nne za mahusiano ambazo ni mahusiano ya kifamilia, mahusiano ya kirafiki, mahusiano ya kimapenzi, na mahusiano ya kawaida ya kufahamiaana tu.

Mahusiano ya kifamilia ni yale ambayo yanatokana na undugu wa damu au kufahamiana kati ya mtu mmoja na mwingine au familia moja na nyingine. Mfano:, Kama mmezaliwa wawili katika familia moja basi nyie mtakuwa na mahusiano ya kindugu kwani mmeunganishwa na damu zenu na ni familia moja. Kama kuna familia mbili tofauti lakini wapo karibu Kama ndugu basi na wao wanaingia katika uhusiano huu mfano:, familia ya shayo wana uhusiano na familia ya mwakasege hii inaonesha ni watu ambao hawaungani kwa damu lakini wanafahamiana kwa muda, wanashirikiana pamoja na wamekuwa kama ndugu. Huu ni uhusiano wa kawaida ambao mara nyingi watu wanaweza kuuelewa.

Mahusiano ya kirafiki ni yale yanayotokana na mtu na mtu kuwa karibu, wakishirikiana pamoja katika mambo mbalimbali maishani mwao, na ukaribu huo unaweza kuwepo kwasababu aidha walisoma pamoja, au wamekuwa pamoja tangu utotoni, au wanafanya kazi pamoja. Uhusiano wa kirafiki hauishii kwa ngazi ya mmoja tu hapana, hata nchi na nchi zinaweza kuwa marafiki kutokana na historia zao. Mfano:, nchi yetu Tanzania ina uhusiano wa kirafiki na nchi kama Malawi, Msumbiji n.k ni kutokana na historia walizonazo pamoja, pia ujilani wao.

Mahusiano ya kufahamiana tu, haya huja pale unapokuwa na mtu ambaye hamna historia yoyote pamoja lakini mmefahamiana hivi karibuni kutokana na tukio fulani au aina yoyote ya mazingira yaliyojitokeza, uhusiano huu ni ule usio wa ndani kwasababu pande zote mbili hazijuani kwa kina na wala hawashirikiani sana kama kwenye aina zingine za mahusiano. Mfano:, inaweza kutokea unamfahamu mtu na una namba yake ya simu lakini hampo karibu sana kama inavyohitajika na pengine mnawasiliana tu pale inapohitajika kufanya hivyo.

Aina ya mwisho ni uhusiano wa kimapenzi, huu ni uhusiano baina ya watu wawili (mara nyingi ni jinsia mbili tofauti) ambao unawaunganisha kihisia, kiakili na kimwili. Uhusiano huu umebeba hisia kali za kimapenzi yaani kuhisi upendo kwa mtu kiasi kwamba mtu huyo anatawala mwili na mawazo yote na kuona hata maisha hayana maana bila uwepo wa mtu huyo. Ni uhusiano ambao kwa mara nyingi ndio unazungumziwa sana kwani umebeba mambo mengi na ndio wenye nguvu sana. Mahusiano yote yaliyotajwa hapo juu yana husisha sana akili na hisia za watu lakini aina hii ya mahusiano yanaongeza kipengele kingine cha kimwili nikimaanisha pengine hawa wawili wanagusana kimwili na hata kufanya ngono (tendo la ndoa) kujiridhisha na kukamilisha matamanio yao na uhusiano wao.

Mahusiano yote yanaweza kuwa chanya au hasi kulingana tuu na vile mahusiano hayo yanavyo endeshwa. Aina hizi nne za mahusiano ndizo zinaleta aina zingine zote za mahusiano zinazo julikana huko nje mfano:, mahusiano ya kibiashara yanaweza kutokea aidha unamfahamu mtu kirafiki, kifamilia, kimapenzi au mmefahamiana tu kawaida kwa siku moja.

Ili mahusiano yaweze kusimama na kuonekana yapo hai kuna sheria, matakwa, mipaka ya kimaamuzi na mitazamo ya pamoja ambayo huwekwa kuhakikisha mahusiano hayo yanafanikiwa, na kama mambo hayo hayafatwi au kuwekwa kipaumbele basi mahusiano hayo yatavunjika na itakuwa ngumu kuyaendesha. Pia ninaamini uhusiano wa nchi yetu na nchi zingine katika jumuiya ya Afrika mashariki pia una sheria na mipaka ambayo katika hiyo jumuiya hii imesimama. Vivyo hivyo hata uhusiano wa kimapenzi unafata taratibu zote kama uhusiano mwingine.

Usikose kuungana nami sehemu inayofuata........!

imeandaliwa na mwandishi Samwel Dihigo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...