Ruka hadi kwenye maudhui makuu

DHAMBI YA MAAGANO (LAANA YA UKOO) part 02


 Pamoja na Late, Mwl. Godwin Dihigo.

JE MTU ANAWEZA KURITHI DHAMBI?

Kila mkristo anapaswa kuiga mfano wa watu wa Beroya. Watu hawa wa Beroya Paulo aliwasifu sana kwa hekima yao ya kutokuamini jambo bila kulichunguza. Hawakuona kuwa ni busara kumuamini Paulo eti kwa sababu ni mtume bali waliyachunguza yale asemayo kama yalikuwa sahihi.

 

Tunasoma ukweli huo katika Matendo 17:10-12

Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya nao walipofika huko wakaingia katika Sinagogi la Wayahudi. Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike kwa kuwa waliyachunguza maandiko kila siku waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. Basi wengi miongoni mwao wakaamini na wanawake wa Kiyunani wenye cheo na wanaume si wachache.

 

Ukisoma kwa makini mlango huu utagundua kuwa kuna watu wa aina mbili.

 

1. Wale wa Thesalonike na

2. Wale wa Beroya

 

Lakini Paulo anawasifu watu wa Beroya kwa kuyachunguza maandiko. Si kila kitu anachosema mwanadamu katika neno la Mungu ni ndiyo bila kupata ushahidi wa biblia au neno la Mungu. Pata ushahidi muulize vizuri Yule anayekufundisha ili ujiridhishe upate kushinda.

 

Watu wa Thesalonike uwenda wako kama watu wa leo wanaopelekwa pelekwa kwa maneno ya uongo kutoka kwa manabii wa uongo. Kwa sababu hawataki kusoma biblia pia hawataki kufundishwa na waalimu waaminifu wa neno la Mungu kutoka kanisa la Kristo. Waliamini waliyosema .

 

Mungu anasema hakuna Mwanadamu yeyote anayeweza kurithi Dhambi ya mtu mwingine.

 

Katika Ezekiel: 18:1- 4 tunasoma hivi:

Neno la Bwana likanijia tena kusema je! Maana yake nini hata mkatumia mithali hii katika Esraeli, mkisema Baba wamekula Zabibu mbichi nao watoto wakatiwa ganzi ya meno? Kama mimi niishivyo asema Bwana Mungu hamtakuwa na sababu ya kutumia tena mithali hii katika Israeli Tazama Roho zote ni mali yangu kama vile Roho ya Baba ni mali yangu vivyo hivyo Roho ya Mwana mali yangu, Roho ile itendayo Dhambi itakufa.

 

Katika mstari wa 20 Mungu anaendelea kusema

 

Roho itendayo Dhambi ndiyo itakayokufa Mwana hatauchukua uovu wa Baba yake wala Baba hatauchukua uovu wa Mwanawe. Haki yake mwenye haki itakuwa juu yake na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.

 

Je kurithi Dhambi ya ukoo kunatokea wapi? Je hujagundua kuwa huo ni mpango wa Wachungaji wa kujipatia fedha? Hayo tunayosoma hapo ni maneno ya Mungu yaliyowaonya wanadamu wa wakati ule kuwa hakuna mtu awezaye kurithi Dhambi ya mtu mwingine.

 

Mungu akiendelea kusema, akamuagiza Musa awaambie wana wa Israeli juu ya watoto kurithi zambi ya Wazazi wao si fundisho sahihi akasema hivi katika Kumb: 24:16

 

Mababa wasiuawe kwa ajili ya Watoto wao, wala Watoto wasiuwawe kwa ajili ya Baba zao kila mtu na auawe kwa Dhambi yake mwenyewe.

ITAENDELEA..................

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...