Na late, Mwl. Godwin Dihigo.
Katika
kitabu cha Muhubiri sura ya 7:29 tunasoma maneno haya;
“Tazama
hili tu nimeliona, Mungu amemfanya mwanandamu mnyofu lakini wamebuni mavumbuzi
mengi”
Sijawahi
kusoma mahali popote katika biblia panaposema mtu aliyeokoka kweli kweli
uwokovu uliyo sahihi anaweza kubaki na laana ya maagano ya ukoo.
Tena
si yake yeye mwenyewe bali ya mababu na mabibi waliyoagana nayo zamani.
Sijawahi kusoma maneno ya Mungu yanayosema mtoto anaweza kurithi dhambi ya baba
na mama yake au niseme dhambi ya ukoo wao. Haya ni maneno ya kutegenezwa na
wachungaji ili wajipatie faida.
Mungu
alijua hili, ndiyo maana alituonya mapema
Tunasoma
katika 2 Petro 2:1-3 maneno haya
“Lakini
waliondokea manabii wa uongo katika wale watu, kama vile kwenu watakavyokuwako
walimu wa uongo watakaoingiza kwa warevu, uzushi wa kupoteza wakimkana hata
Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia. Na wengi watafuata ufisadi
wao na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. Na katika kutamani watajipatia faida kwenu
kwa maneno yaliyotungwa ambao hukumu yao tangu zamani haikawii wala uvunjifu
wao hausinzii”
Mungu
anatujulisha kuwa fundisho la mkristo kupata laana ya ukoo ambao mababu na
mababa waliagana na mizimu halina nafasi kwa wale wote waliookoka na kuwa ndani
ya Yesu. Hawa ni manabii na walimu wa uongo, ambao kwa maneno yao ya kutunga
ili wajipatie faida, hukumu yao haiko mbali.
Wale
wote waliyo ndani ya Kristo, wale waliyookoka wokovu halisi usiyotungwa, Mungu
anasema:
“Hata
imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya yakale yamepita, tazama
yamekuwa mapya. 2 Kor 5:17.
Je
wewe usomae ujumbe huu umeokoka wokovu halisi?, kama ndiyo hiyo dhambi ya ukoo
nani ameibakiza ikiwa damu ya Yesu imekusafisha katika maji ya ubatizo?.
Wachungaji
na waalimu wengi wanaofundisha fundisho hili hawakusoma kwamba hakuna mtu
anayerithi dhambi ya mtu mwingine?. Nini kinachowasumbua hata wasiwaambie
wanadamu wenzao ukweli?
Na
hii yanadhihirisha maneno ya mungu katika kinywa cha mtumishi wake Paulo. Mtume Paulo akiwaonya wakristo wa Rumi juu ya
watu wajiitao manabii, wachungaji waliyojiita wenyewe na walimu wa uongo
waletao mafundisho ya kutungwa akasema:
“Kwa
sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe na
kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu Rumi 16:18”.
Je
umemuelewa vizuri Mungu kupitia mtumishi wake Paulo?, utapataje laana ya ukoo
iwapo wewe umeokoka?, je huyo mwalimu wako na mchungaji wako bado unamwamini?
Mungu
hakuongea hilo kwa warumi tu, bali alimtuma Paulo aseme na wafilipi
waliyookoka. Tunasoma haya katika Filipi 3:18-20
“Maana wengi uenenda ambao nimewaambieni habari zao na sasa nawaambia hata kwa machozi kuwa ni adui wa msalaba wa kristo mwisho wao ni uharibifu, Mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedhaha yao waniao mambo ya duniani. Kwa maana sisi wenyeji wetu uko mbinguni”.
Mungu
anasema watu wote waletao mafundisho ambayo Mungu hakuagiza, hawa wanafanya
kazi ya Mungu wao wenyewe ambaye nitumbo.

Maoni
Chapisha Maoni