Maswali 26 ya Kimahaba Kusaidia Mioyo
Iliyokaribia Kusahau Mapenzi.
Utangulizi: Upendo Huumiza Kimya Kimya… Tiba
Huwaponya Waliochoka Kupendwa
Katika kila ndoa, kuna mambo ambayo
hayatamkwi, lakini yanahisiwa. Kuna siku moja utamwangalia mwenzi wako na
usione tena yule uliyekuwa ukimtamani kwa macho ya kiu na moyo wa shauku. Si
kwa sababu hampendani tena, bali kwa sababu maisha yamewabeba mbali na mlipoanzia.
Ndoa si ndoto tamu kila siku. Kuna siku
mtacheka hadi machozi yawatoke, lakini pia kuna siku mtalala migongo ikiwa
haijaambiana neno. Watu hubadilika.
Mioyo huumia. Mazoea huua msisimko wa mapenzi. Na hapo ndipo tiba ya
mapenzi inapohitajika. Si kwa sababu upendo umeisha, bali kwa sababu upendo
unahitaji kupaliliwa kama maua bustanini.
Ndiyo maana kila baada ya miaka miwili, wanandoa wanapaswa kupiga breki, kuketi
kimya, na kuulizana maswali yanayogusa
roho, si akili. Maswali ambayo hufungua milango ya mawasiliano,
hukumbusha ahadi, huchambua madonda na pia huamsha shauku mpya.
Hii ndiyo TIBA YA MAPENZI, njia ya kipekee ya kurejesha moto, kuboresha
mawasiliano, na kujenga msingi wa kudumu wa mahaba.
Kanuni 5 za Love Therapy (Kabla ya Kuingia
Moyoni, Elewana Nia)
- Kuwa muwazi
na mkweli. Hii si fursa ya kujitetea – bali
kujieleza.
- Jibu kwa
maandishi, na kwa hisia. Andika kwa
moyo, si kwa kalamu pekee.
- Mkishamaliza,
badilishaneni majibu.
Kabla ya kusoma… chukueni busu la
upendo – lile la kunyamazisha dunia.
- Soma majibu
ya mwenza wako kwa sauti. Hakikisha
anasikia uchungu wako, furaha yako, na matarajio yako kupitia sauti yako.
- Zungumzieni
kila jibu.
Pale kwenye maumivu, pigeni magoti ya maelewano. Pale kwenye furaha,
shikeni mikono ya shukrani.
💖
Maswali 26 ya Tiba ya Mapenzi: Kila
Swali ni Dawa ya Mahusiano
- Ni kitu gani
kilikufanya ukamchagua mwenza wako, kuwa wako?
- Wakati
mnavalishana pete, malengo yako ya ndoa yalikuwa yapi?
- Ni nini
katika ndoa yako hakikupi furaha kwa sasa?
- Ni mambo
gani yanayokufanya utabasamu ukifikiria ndoa yako?
- Ukipewa
nafasi ya kuibadilisha ndoa yako, ungefanya nini?
- Unahisi
namna gani Mungu anahusika au kuheshimiwa katika ndoa yenu?
- Unazungumziaje
hali yenu ya mawasiliano? Ina ladha gani?
- Mnapataje
maamuzi kwenye mambo muhimu yenu wawili?
- Mnashughulikiaje
migogoro yenu? Mnagusana au mnagusanisha hasira?
- Elezea hali
ya maisha yenu ya kiroho/imani kama wanandoa.
- Kuna ndoa
nyingine inayowapa hamasa? Kipi kinavutia kutoka kwao?
- Changamoto
kubwa mnayopitia ni ipi kwa sasa?
- Ni kitu gani
kimeifanya ndoa yenu isimame mpaka leo?
- Ni mapungufu
gani umeyaona ndani ya ndoa yenu?
- Mnahitaji
kufanya nini ili ndoa yenu ipige hatua nyingine ya kimapenzi na uelewano?
- Elezea picha
ya ndoa ya ndoto zako – ile inayokufanya ukose usingizi wa furaha.
- Ni nini
mwenza wako anaweza kufanya kuboresha ndoa yenu?
- Ni matatizo
yapi unayodhani yametokana na makosa yako mwenyewe?
- Unadhani
Mungu anafanya nini juu ya ndoa yenu sasa hivi?
- Ni kikwazo
gani huwa kinawarudisha nyuma katika kusuluhisha tofauti zenu?
- Ndoa yenu
imebadilikaje tangu muoane – nzuri zaidi au imepungua ladha?
- Mwenzi wako
akikukwaza – huwa unafanya nini?
- Unaonaje
tendo la ndoa kati yenu wawili?
- Unatosheka
na tendo la ndoa? Kama hapana, unahitaji nini kifanyike?
- Elezea eneo
moja linalowasumbua katika ndoa yenu. Tatizo ni nini na suluhisho linaweza
kuwa lipi?
- Unamuoneshaje
mwenza wako upendo na shukrani? (Love language yako ni ipi?)
Mwisho wa Safari, Mwanzo Mpya wa Mapenzi
Kila swali ni mto wa kujitazama ndani ya macho
ya mpenzi wako, si kama mama au baba wa watoto wenu, bali kama yule mpenzi aliyekufanya uone dunia ikiwa na
rangi mpya. Zoezi hili halihitaji pesa wala zawadi, linahitaji muda, hisia,
na ukaribu wa kiroho.
Washa mshumaa, weka muziki wa taratibu,
mvaliane kama siku ya kwanza mlipokutana. Andikeni kwa mikono yenu, sobaneni
kwa mioyo yenu, na busuaneni kwa ndimi
zenu zenye shukrani.
Ndiyo tiba hii.
Ndiyo mapenzi haya.
Ndiyo ndoa hii.
Na bado mna nafasi ya kuifanya kuwa
bora zaidi.
Maoni
yako ni ya muhimu!
Umeshajaribu tiba
ya mapenzi kama hii? Je, ungependa kuipitia na mwenza wako? Tuambie kwenye
comment hapa chini, au shiriki makala
hii na wapendwa wengine wanaoitafuta nuru ndani ya ndoa zao.

Maoni
Chapisha Maoni