Ruka hadi kwenye maudhui makuu

“Alivyolala na Bestie Wake – Siri ya Mapenzi ya Emma”


 Jina langu ni Emma… Niliamini mapenzi yanaweza kuponya kila jeraha, kuleta furaha, na kunifanya nijisikie salama.

Nilikutana na Franklin kwenye sherehe ya kumbukumbu ya siku y kuzaliwa ya rafiki yangu. Alikuwa mkarimu, mwenye mzaha, baada ya kupeana namba za simu, kila asubuhi alikuwa ananiamsha kwa mahaba na kiukweli alifanya hali ya hewa ya moyo wangu kuwa ya kiutukufu.
Tulianza kuonana. Kunywa juice. Kucheka bila sababu. Nikajikuta nimeanguka kwenye mapenzi.

Katika mahusiano yetu Siku moja alinijulisha kuna mtu maalum sana kwake. Bestie wake. Anaitwa Jackline., akisema ni msichana anayefahamiana naye kwa muda na ni marafiki tu wa karibu. Sikumpenda jackline lakini hakuwai nipa sababu ya kuhisi kama kuna kitu kati yao.

Mara nyingi mpenzi wangu aliniaga na kusema:
"Baby niko kwa Jackline leo, tunapika chapati na kusikiliza mziki. Huyu bestie wangu anakujua sana, kila kitu anakutetea."


Niliamini. Kila mara alipokuwa kwa Jackline, nilihisi wivu… lakini nikakumbuka, "Ni bestie tu."


Siku moja, nikiwa nyumbani kwa Franklin, tulishinda pamoja nikafanya usafi wote wa nyumba yake, nikapika tukala wote, kisha nikaondoka. Bahati mbaya nilisahau simu yangu. hivyo Nilirudi usiku kuichukua bila kusema.


Niliingia kimya kimya kutaka kumshtua mpenzi wangu kama utani. Milango ilikuwa wazi. Mziki wa taratibu ukisikika. Nilifikiri amelala na kupitiwa

Lakini kilichofuata… kilinivunja zaidi ya ajali yoyote.


Nilimwona… Franklin. Na Jackline. Sio kwenye sahani ya chapati. Bali kwenye shuka walizojifunika pamoja.

Kwa hasira nikamwita na kusema:
"Franklin…? Huu ni utani gani…?"

Franklin kwa kutahamaki na hofu akajibu:
"Emma! Sio vile unavyofikiria… Samahani"

Jackline kwa kutaka kuufunika ukweli akasema:
"Emma, si unajua ni bestie tu, hii ni bahati mbaya…"


Nilianguka sakafuni. Machozi hayakuwa tu ya uchungu… bali ya mshituko.

Niliamini mtu mmoja… lakini alikua na moyo kwa wawili.

Jackline alikuwa rafiki yangu pia. Baada ya kukutanishwa nae na mpenzi wangu franklin. Alikuwa mtu wa karibu sana kwangu. Tulikuwa tukicheka pamoja,kuambiana siri zetu, kila kitu kwa undani kabisa, tulikuwa tunafurahi na kupiga picha pamoja… na sasa, alikuwa amepiga moyo wangu picha ya maumivu.


Sasa ni wiki tatu tangu niondoke kwenye maisha ya Franklin.

Ninajifunza kupenda bila kujiumiza. Kujua kuwa upendo sio kifo, sio kusamehe kila udhalimu kwa jina la "mapenzi."


Lakini swali linabaki…

“Je, kweli kuna ‘bestie’ wa jinsia tofauti bila tamaa ya siri?”
Na kama mapenzi yalianza kwa uaminifu, kwa nini yakome kwa usaliti?”


Je, umewahi kuumizwa kama Emma? Ungependa kushiriki hadithi yako? Tuandikie kwenye comment.
Na kama unataka kujifunza mengi kuhusu siri za mapenzi… subscribe sasa.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Maisha: Safari Yenye Maswali Zaidi Kuliko Majibu

  Karibu sana kwenye blogu yangu! Leo naandika chapisho langu la kwanza – mwanzo wa safari ya mawazo, mazungumzo, na tafakari juu ya maisha. Maisha ni safari isiyo na ramani kamili, na cha kushangaza ni kwamba kila hatua tunayopiga huibua maswali mapya. Tunazaliwa bila kujua lolote, tunaingizwa kwenye mifumo ya maisha – shule, kazi, mahusiano, jamii – tukitarajiwa kuelewa kila kitu kwa haraka. Lakini ukweli ni kwamba, wengi wetu tunaishi tukijaribu kuelewa maana halisi ya maisha, tukitafuta majibu kwenye imani, mapenzi, kazi, au hata burudani. 🔍  Kwa Nini Naandika Blogu Hii? Ninaamini kuwa kila mtu ana hadithi, swali, au wazo ambalo linaweza kumgusa mtu mwingine. Blogu hii ni mahali pa kuzungumza kuhusu yale mambo ya kila siku – yaliyo wazi, yaliyo magumu, na hata yale ya kushangaza ambayo hayasemwi sana. Tutazungumzia imani, mitindo ya maisha, afya, historia, burudani, mapenzi, na yale mambo ambayo huenda hujawahi kuyawaza kabisa. Lengo si kutoa majibu yote, bali kuibua f...

WIVINA SYLIDION: SHUJAA WA MABADILIKO KWA MSICHANA WA KITANZANIA.

 Na Palubongo Team. Katika kona ya kaskazini-magharibi mwa Tanzania, mji wa Bukoba unafahamika kwa mandhari yake ya kuvutia, ziwa Victoria, na watu wenye upendo. Lakini kuna jina moja linang’aa zaidi ya mandhari, jina la msichana kijana, mwenye ndoto kubwa, moyo wa dhati, na kiu isiyozimika ya kuleta mabadiliko: Miss Wivina Sylidion . Alizaliwa na kulelewa Bukoba, mkoa wa Kagera, Wivina alionyesha mapema kuwa safari yake haitakuwa ya kawaida. Akiwa na Shahada ya Sayansi na Elimu, aliamua kutumia elimu yake kama chombo cha ukombozi hasa kwa wasichana walioko kwenye mazingira magumu. Aliona mapema jinsi jamii inavyowatizama wasichana kama dhaifu, na akaapa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Wivina si tu mwalimu wa darasani bali ni mwalimu wa maisha. Kupitia taasisi aliyoianzisha kwa moyo wake mwenyewe “Binti na Kesho Yako” , amekuwa akiwafikia wasichana mashuleni, akiwapa elimu ya afya, maarifa ya kijamii, stadi za maisha, na matumaini. Anaamini kuwa msichana anapojitambua, jamii ...

Pua: Kiungo Kidogo Chenye Nguvu Kubwa Kuliko Tunavyodhani

K una msemo wa Kiswahili usemao, "Usidharau kidogo chenye maana." Lakini kwa bahati mbaya, wengi wetu tumekuwa tukidharau kiungo kimoja cha mwili wetu kwa sababu tu ni kidogo – pua . Tunaizungumzia mara chache, hatuitunzi ipasavyo, na mara nyingine tunaificha au kuifanyia upasuaji kwa sababu hatuipendi jinsi ilivyo. Lakini hebu tusimame kidogo na tujiulize: je, tunafahamu kweli nguvu iliyo ndani ya kiungo hiki kidogo? Tuangalie pamoja nguvu ya pua; 1. Mlango wa Maisha: Kupumua Kila pumzi tunayovuta huanza kwenye pua. Hapo ndipo maisha huingia. Bila hewa, hakuna uhai. Lakini si tu kuvuta na kutoa hewa – pua huchuja vumbi, vijidudu, na hata unyevu wa hewa kabla haijafika kwenye mapafu. Ikiwa tungekosa pua, mapafu yetu yangekuwa kwenye hatari kubwa sana kila tunapopumua. 2. Hisia Zinazoamsha Kumbukumbu Hebu fikiria harufu ya chakula cha nyumbani – labda wali wa nazi, au samaki wa kupaka unaopikwa na mama. Au harufu ya mvua ya kwanza kunyesha ardhini. Au hata manukato ...